23.2 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Taylor Swift ashtakiwa kwa wizi

Taylor_SwiftNEW YORK, MAREKANI

MSANII maarufu zaidi duniani kwenye mtandao wa Instagram, Taylor Swift, ameshtakiwa kwa kuiba mistari ya wimbo wa msanii mwenzake, Jesse Braham na kuutumia katika wimbo wake maarufu wa ‘Shake It Off’.

Jesse alisema wimbo huo aliutunga mwaka 2013, ulijulikana kwa jina la ‘Haters Gone Hate’, hivyo anashangaa kuona baadhi ya mistari katika wimbo wa Taylor.

Iwapo Taylor atapatikana na hatia atatakiwa kulipa faini ya dola milioni 42 na huku mshitaki akitaka jina lake lijumuishwe katika rekodi za wimbo huo kama mtunzi mchangiaji wa wimbo huo.

”Niliusikiliza wimbo huo mara kwa mara na nafsi yangu iliniandama na nikagundua kwamba wimbo huu ni wangu kuanzia mwanzo hadi mwisho,” alisema Braham.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles