30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Tamthilia ya Mama Kubwa mbioni kukamilika

mtitu-3NA GEORGE KAYALA

TAMTHILIA mpya iliyopewa jina la Mama Kubwa inayoandaliwa na Kampuni ya 5 Effects Movies Ltd, ipo mbioni kukamilika baada ya kuandaliwa kwa muda mrefu na kuna uwezekano wa kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu.

Akizungumza na MTANZANIA jana mmoja wa waandaaji hao ambaye pia ni mmiliki wa kampuni hiyo, William Mtitu, alisema anaamini kazi hiyo itakuwa nzuri kwani waigizaji wamejitahidi kuonyesha uhalisia wakati wa kucheza tamthilia hiyo ambayo itakuwa ni ya kufungia mwaka.

“Tupo katika hatua ya mwisho kuikamilisha tamthilia hiyo tuliyoipa jina la Mama Kubwa ambayo naamini itakuwa katika ubora wa hali ya juu kutokana na wasanii walivyoitendea haki wakati wa kuigiza,” alisema Mtitu.

Aidha, Mtitu alisema kuwa kampuni yake ilisimamisha suala la kutoa filamu na tamthilia kwa lengo la kupisha uchaguzi mkuu uliopita kwani akili za wadau wengi zilielekezwa kwenye kampeni za wagombea wa vyama vya siasa hivyo endapo wangetoa kazi zao wangeingia hasara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles