25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Siafu waua bwana harusi

siafu
siafu

Na Ibrahim Yassin, Rungwe

WAKAZI  wa Kijiji  cha  Nditu,  Kata  ya Suma, Wilaya ya Rungwe  mkoani Mbeya, wamegoma  kuzika mwili wa marehemu Shabani  Yusufu (27),  baada kushambuliwa na kundi la  siafu nyumbani kwake  na kusababisha apoteze uhai.

Yusufu, amefariki dunia ikiwa ni siku moja tu baada ya kufunga ndoa na kuzua gumzo kubwa kijijini hapo.

Alikutwa na mauti hayo akiwa amejipumzisha ndani usiku wa kuamkia jana, jambo ambalo linahusishwa na imani za kishirikina.

Akisimulia mkasa huo, baba mzazi wa marehemu, Ebron Mwaipaja, alisema mwanawe  alitoka kufunga ndoa  juzi na alikutwa na mauti hayo akiwa amejipumzisha chini ya mti nyumbani kwake, ambako ghafla alivamiwa na siafu.

Alisema kulikuwa na maneno ya hapa na pale wakati wa maandalizi ya harusi hiyo kutoka kwa baadhi ya watu, ambayo yamesababisha tukio hilo kuhusishwa na imani za kishirikina.

Baba huyo alisema baada ya tukio hilo, wananchi na uongozi wa Serikali ya kijiji walifika eneo hilo, huku wakimtaja mmoja wa wanakijiji kuwa ndiye “aliyetuma” siafu hao.

“Wananchi waligoma kuandaa taratibu za mazishi wakishinikiza aletwe mganga wa jadi apige ramli ili kumbaini mtu anayeendesha matukio ya ushirikina yanayoendelea kijijini hapa,” alisema.

Alisema baada ya wananchi kugoma kuzika, Serikali ya kijiji nayo iligoma kutoa kibali, ikisema siku zote Serikali haiamini uchawi, jambo ambalo lilisababisha wananchi waliokujwa na silaha za jadi, kufanya maandamano na kufunga barabara.

Baada ya hali ya usalama kuzidi kuwa mbaya, polisi walifika eneo la tukio na kutuliza ghasia, huku familia ikifanya maandlizi ya maziko bila wanakijiji kuhusika.

“Kijana wangu ndiyo kwanza alitoka kufunga ndoa akifurahia maisha ya kuwa na mke, amekutwa na umauti tena kwa kuvamiwa na siafu wakati kijiji hiki hakijawahi kuwa na wadudu hawa, yote namwachia Mungu,” alisema Mwaipaja.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake, Joseph Kajura, alisema wanafahamu fika tukio hilo ni la kishirikina na ndiyo maana walimtafuta mganga wa kienyeji ili apige ramli kwa ajili ya kubaini mhusika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles