24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Rose Ndauka amwaga ajira kwa vijana

Na Brighiter Masaki

MSANII wa filamu nchini, Rose Ndauka ametoa ajira kwa vijana wenzake baada ya kufungua saluni ya kike na kiume inayotoa huduma hadi kwa watoto iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar Es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Ndauka amesema kuwa sio kitu rahisi kwani alijipanga kwa muda mrefu katika kufungua biashara hiyo na kufikiria kutoa ajira kwa vijana wenzake.

“Namshukuru Mungu na wazazi wangu kwa ushiririkiano walionipa kufanikisha kitu kama hiki. Nimefungua saloon ambayo ukija na familia yako mnapata huduma zote kuanzia baba, mama na watoto pamoja na maharusi na shughili nyingine,” amesema Ndauka

Akizungumzia uzinduzi huo, Anty Ezekiel ambaye ni msanii mwenzanke na Ndauka, alimpongeza Rose kwa hatua aliyopiga katika kufungua biashara hiyo kubwa na nzuri ambapo mtu akifika anapata huduma zote kulingana na mahitaji yake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles