Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko wa pili kutoka kushoto akiwaongoza wadau wa TACAIDS kuweka shada la maua kwenye kaburi la Renatus M. Kihongo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Program Maalum- TACAIDS. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Ndugu Yasin Abas akifuatiwa na Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la watu wanaoishi na VVU (NACOPHA), Vitalis Makayula pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa NACOPHA, Deogratius Rutatwa
mazishi yamefanyika Oktoba 20, 2022 jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko akisaini kitabu cha maombolezo katika msiba wa Renatus M. Kihongo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Program Maalum – TACAIDS. Mazishi ya Kihongo yamefanyika Oktoba 20, 2022 Dar es Salaam.Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la watu wanaoishi na VVU(NACOPHA), Deogratius Rutatwa akisaini kitabu cha maombolezo katika msiba wa Renatus M. Kihongo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Program Maalum – TACAIDS. Shughuli za mazishi zimefanyika Oktoba 20, 2022 jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS,) Dk. Leonard Maboko akitoa salamu za pole kwa niaba ya Kamisheni na Menejimenti ya TACAIDS katika msiba wa Renatus M. Kihongo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Program Maalum – TACAIDS.Sehemu ya waombolezaji.