24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

PAC YASHTUSHWA NA MTAJI WA 150,000 WA MWEKEZAJI MLIMANI CITY

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kamati hiyo pia imeelezwa kuwa mwekezaji katika mradi wa uwekezaji wa Mlimani City alikuja na mtaji wa Dola za Marekani  75 (Sh 150,000) kuwekeza katika mradi huo.

Kamati hiyo ambayo iko katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali pia imebaini madudu katika mradi huo na kuagiza wote waliosaini mkataba huo waitwe na kuhojiwa.

Aidha, kamati hiyo imeshangazwa na hatua hiyio na kuhoji taaaisi kubwa kama ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ( UDSM) inayoaminika ndani na nje ya nchi ilishindwaje kukopa fedha za kuendesha mradi huo hadi kukubali mwekezaji wa aina hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Naghenjwa Kaboyoka, amesema kuna vitu vingi vimejificha katika mkataba huo hivyo ni lazima kuwe na watu  watakaowajibika.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye amekiri mkataba huo kuwa na matatizo hivyo wanachukua hatua kuyatatua.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Utawala, Profesa David Mfinanga, amesema wameunda kamati kupitia upya mkataba huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles