24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Nyota watatu kung’oka Simba

SimbaNA JUDITH PETER, DAR ES SALAAM

TIMU ya Simba imepanga kuwatema nyota wake watatu na kusajili wachezaji wenye uzoefu ili kuimarisha kikosi hicho ambacho kinaundwa na chipukizi wengi.

Simba imeanza mikakati ya usajili kwa ajili ya msimu ujao baada ya kumaliza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu ikiwa nafasi ya tatu huku ubingwa ukinyakuliwa na watani wao wa jadi Yanga na Azam kushika nafasi ya pili.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi Ofisa Habari wa timu hiyo, Haji Manara, alisema uongozi unasubiri ripoti ya kocha wa timu hiyo Mserbia, Goran Kopunovic, ili zoezi la usajili liweze kufanyika kwa kufuata mapendekezo yake.

Alisema pamoja na Simba kumaliza ligi ikiwa nafasi ya tatu, bado wanaamini wachezaji wao wana viwango na ubora unaokubalika hivyo hawana mpango wa kufanya mabadiliko makubwa kwa ajili ya msimu ujao.

Alisema ripoti ya Kopunovic inayotarajiwa kukamilika mapema wiki hii, ndiyo itatoa mwongozo kwa Kamati ya Usajili ya Simba inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Zacharia Hans Poppe kama wachezaji watakaoongezwa ni wa kulipwa au wazawa.

“Wapenzi wa Simba wasitarajie mabadiliko makubwa katika usajili kwani timu hii itaendelea kuwepo na wachezaji watakaoachwa hawawezi kuzidi watatu na watakaosajiliwa itategemea mapendekezo ya kocha,” alisema.

Wakati huo huo, Kopunovic alielezea kufurahishwa na ushindi walioupata wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Ruvu katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku akidai matokeo hayo yamedhihirisha ubora wa kikosi hicho kwa msimu huu.

Alisema wachezaji walicheza kwa kujituma na kumfanya ajivunie kikosi bora licha ya kuzidiwa mbinu na watani wao wa jadi, Yanga na kushindwa kutwaa ubingwa msimu huu.

Simba iliyomaliza ligi kwa kujikusanyia pointi 47 imekosa nafasi ya kuiwakilisha Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika mwakani baada ya kuzidiwa kete na Azam iliyomaliza kwenye nafasi ya pili.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles