27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

NMB yajipanga kusaidia kufufuliwa zao la Mkonge nchini

Na Mwandishi Wetu, Tanga

Benki ya NMB imesema kuwa itahakikisha inaendelea kutoa huduma za kifedha kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kufufua zao la Mkonge na kuboresha uchumi wa wakulima wa zao hilo nchini.

Hatua hiyo inakuja baada ya serikali kuanza mikakati ya kuhakikisha zao hilo linafufuliwa na kuwanufaisha wakulima na taifa kwa ujumla kama ambvyo ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Akiongea mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa kikao cha wadau wa Mkonge kilichofanyika jana Mkoani Tanga, Ofisa Mkuu wa wateja binafsi  na biashara wa Benki hiyo, Filbert Mponzi, alisema kuwa NMB itaendeleza jitihada za kufufua zao hilo ambazo imezianza.

Alisema kuwa tangu serikali imeanza kulifufua zao hilo benki hiyo imekuwa ikitoa ushirikiano ambapo imetoa zaidi ya bilioni 1 kwa ajili ya ununuzi wa matrekta 11 na trela 22 vifaa ambavyo vitapunguza gharama ya uendeshaji na kuongeza tija na pato la wakulima wadogo wa mkonge.

Afisa Mkuu wa wateja Binafsi na Biashara wa benki ya NMB, Filbert Mponzi akizungumza katika mkutano wa wadau wa zao mkonge uliofunguliwa na Waziri Mkuu , Kassim Majaliwa jijini Tanga.

Aidha, aliongeza kuwa Benki hiyo imeendelea kutoa mikopo ya pembejeo na uendelezaji wa mashamba ya Mkonge kwa wakulima wadogo, kati na wakubwa ili kuongeza uzalishaji na mapato ambapo zaidi ya Sh bilioni 6 zimeshatolewa kwa wakulima wa mkonge.

Alisema kuwa NMB imefanikisha kufungua akaunti kwa wakulima zaidi ya 1,500 ambapo akaunti hizo zinajumuisha wakulima mmoja mmoja na wale wanaozalisha kupitia Vyama vya msingi.

“Uwepo wa akaunti hizi unajenga utamaduni wa wakulima kutumia huduma za benki kwa usalama wa fedha zao na mazingira sahihi katika kupata huduma zaidi ya kifedha ikiwemo Mikopo.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu ili kuendelea kuwajengea uwezo wakulima wadogo na kupata mitaji NMB kupitia taasisi kanzu ya NMB Foundation inaendelea kutoa mafunzo kwa wakulima kupitia vyama vya vya msingi na kikundi ili kuimarisha utendaji na kuongeza soko,” alisema Mponzi.

Mponzi alibainisha kuwa Benki ya NMB itaendeleza jitihada hizo, ikiwemo kutoa mikopo mikubwa, midogo na ya kati ili kuhakikisha wakulima wa zao wanazlisha kwa tija.

“NMB tutaendelea mikopo katika ngazi zote za uzalishaji wa zao la mkonge, ikijumuisha mikopo ya muda mfupi na muda wa kati (yaani uwekezaji). Mikopo hii inajumisha pembejeo, upanuzi na miundo mbinu ya mashamba, matrekta, mashine za uchakataji wa mkonge, viwanda vya mkonge pamoja na huduma mbalimbali katika sekta,” alisema.

Akizungumza katika kikao hicho cha wadau wa zao la Mkonge, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema kuwa mpaka kufikia mwaka 2025 Tanzania inatarajia kuzalisha tani 120,000 za Mkonge kwa mwaka.

Majaliwa alisema kuwa zao la Mkonge ni miongoni mwa mazao ya biashara hapa nchini ambayo mikakati yake ilitekelezwa vizuri itawezesha serikali kupata fedha za kigeni lakini pia kukuza pato la mwananchi mmoja mmoja.

“Kilimo cha zao la Mkonge na mchikichi unatuondolea mzigo mkubwa sana kwa kupunguza gharama mfano baada ya kuhamasisha kulima mchikichi tunaokoa zaidi dola za marekani 470 milioni za kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi,” alisema Majaliwa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema kuwa kwa sasa Wizara tayari imeshatenga shilingi Bilioni 175 kwa ajili ya kufanya utafiti ili kuzalisha mbegu bora na zenye gharama nafuu.

Bashe alisema kuwa Wizara imeweza kuandaa utaratibu wa hati ya dhamana (LC) utakaowezesha wakulima wadogo kuchukua mkopo kwenye taasisi za fedha kwa riba ya asilimia mbili tu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles