30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

NANDY AANZA KUPATA DILI KIMATAIFA

Na JESSCA NANGAWE-DAR ES SALAAM


MREMBO anayefanya vyema na ngoma ya Kivuruge, Faustine Charles ‘Nandy’,  ameanza kupata ofa za kufanya shoo za kimataifa.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Nandy ambaye alisema kwa kipindi kirefu alikuwa akitamani kupata nafasi ya kufanya shoo nje ya nchi, sasa anaona matunda ya kazi zake baada ya kupokea mialiko kadhaa kutoka nchi mbalimbali.

“Ni sehemu ya ndoto niliyoitamani kwa muda mrefu, unajua watu wanapoona kazi zako zinafanya vema, hapo ndipo mwanzo wa mafanikio uonekana, nashukuru wengi wameliona hilo na sasa hata mialiko nimeanza kuipata ya ndani na nje ya nchi,” alisema Nandy.

Alieleza  kuwa huu ni mwaka wake wa kuhakikisha anafanya vizuri kimataifa, kwani tayari amejiwekea misingi mizuri hapa nyumbani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles