27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Mwana FA: Wakali wangu ni Sarkodie na 2face

Mwana FANA GLORY MLAY

MSANII anayetamba na wimbo wa ‘Asanteni kwa kuja’, Hamis Mwijuma ‘Mwana FA’, amedai kwamba wasanii wa nje anaotamani kurekodi nao ni mkali wa hip hop kutoka Ghana, Sarkodie na Innocent Ujah Idibia ‘2face’ wa Nigeria.

Alisema wasanii hao ndio wanaomvutia kwa muziki wanaoufanya huku akidai kwa 2fade Idibia anapenda sauti yake anavyoitumia katika muziki wake.

“Nikitaka kurekodi na wasanii wa nje ni hao niliowataja kwa kuwa ndio bora kwangu kwa kuimba na kila kitu kuhusu muziki na si kutoka Afrika Kusini ama Marekani ni Ghana na Nigeria,” alisema Mwana FA.

Mwana FA kwa sasa ana mipango mingi ya kuendeleza muziki wake na muziki kwa ujumla kwa kuwa anataraji kutoka na ‘project’ kubwa na yenye tija kubwa katika muziki wa Tanzania.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles