29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Muhogo Mchungu: Tumieni Kiswahili kwenye kazi zenu

Muhogo Mchungu
Muhogo Mchungu

NA BEATRICE KAIZA,

MKONGWE wa filamu nchini, Abdallah Mkumbila ‘Muhogo Mchungu’, amewataka wasanii wa Tanzania watumie lugha ya Kiswahili katika kazi zao badala ya kutumia lugha ya Kiingereza ili waikuze lugha hiyo

Mwigizaji huyo alisema hayo juzi alipotembelea Ofisi za Kampuni ya New Habari (2006) Ltd wazalishaji wa magazeti ya Bingwa, Rai, Dimba na Mtanzania zilizopo Sinza Kijiweni jijini Dar es Salaam.

“Kazi zetu zinaangaliwa dunia nzima na sisi wasanii ndio tunatakiwa kuwa mstari wa kwanza kusaidia kuikuza lugha yetu kama tunataka nyumba bora ni lazima tuanze na msingi bora, ili lugha ya Kiswahili izidi kusonga mbele tunatakiwa kuitumia zaidi katika kazi na kuacha kutumia lugha za kigeni,” alisema mwigizaji huyo anayetarajia kucheza katika filamu mpya ya ‘Masomo’ pamoja na waigizaji wakongwe, Mzee Majuto na Mzee Korongo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles