28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Charly Confort kutoka Ufaransa kuachia ‘My First Love’ Septemba 4

Paris, Ufaransa

MIONGONI mwa wasanii wanaofanya vizuri kwa sasa nchini Ufaransa ni Charly Comfort ambaye kwa sasa anajiandaa kuachia kazi yake mpya inayoitwa My First Love.

Comfort mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), amefanya mahojiano haya na mtanzania.co.tz ili mashabiki kutoka Tanzania na popote pale duniani muweze kumfahamu vizuri.

Swali: Charly Confort ni nani?

Charly: Mimi ni msanii, mwanamuziki na mjasiriamali. Nilizaliwa Kinshasa nchini DRC kutoka familia kubwa ambayo mimi ni mkubwa.

Swali: Kitabia Charly ni mtu wa namna gani?

Charly: Mimi ni mtu mkarimu, mwenye maamuzi ambaye sipendi kukata tamaa, napenda kufanya mambo mazuri na ninapoanza jambo lazima liende mpaka mwisho.

Swali: Je shauku ya kufanya muziki ilikujiaje?

Charly: Nimekulia katika tasnia ya muziki. Tulipokuwa wadogo, tulifanya muziki aina ya tamtams na marafiki zetu na kila saa 12 jioni tulicheza muziki kwenye mtaa wetu na majirani. Kukua siku zote nilikuwa na hamu ya kuingia rasmi ndani ya muziki lakini nilikuwa nikingojea wakati sahihi.

Nilipofika Ufaransa nilikutana na wasanii kama Modogo Gian, Franco Ferre ambaye alifanya kazi na Papa Wemba na msanii Celeo Scram ambaye alifanya kazi na WerraSon ndipo nilipojifunza jinsi muziki unavyofanya kazi.

Kwa hivyo mwenyewe niliamua kuanza na mtindo wa Afro Beat Love uliochanganywa na rhumba na ndombolo.

Swali: Kwa nini ulichagua kuifanya Afro Béat iliyochanganywa na rhumba na ndombolo?

Charly: Nilichagua hii kwa sababu niliamua kufanya kitu tofauti kwa kuleta mguso wangu wa kibinafsi, ndiyo sababu niliita mtindo wangu AfroConfort.

Swali: Leo katika ulimwengu wa muziki wa Kongo huko Ufaransa na Kongo kuna vijana wengi ambao wanafanya vizuri kama Innos’b, Gaz Mawete, Gaz Fabulous hawakupi changamoto yoyote?

Charly: Kwa hilo nitajibu kwa mfupi. Mimi nafanya muziki wenye mguso binafsi na ninaruhusu hakimu ambaye ni mashabiki waamue kwasababu wao ndio wanafanya twende juu au tushuke chini.

Swali: Jina la kazi yako mpya ni lipi?

Charly: Inaitwa My First Love na kwa Kifaransa ni Mon 1ere amour.

Swali: Kwanini My First Love?

Charly: Kwa kweli nilichagua jina hili kwa sababu mimi mwenyewe napenda muziki mzuri, napenda muziki. Kwa kuwa hii ndio EP yangu ya kwanza kabisa kwenye soko nikachagua jina My First Love.

Swali: Kuna nyimbo ngapi kwenye EP hii ya My First Love?

Charly: Sikutaka kuzindua wimbo mmoja kwa sababu nilitaka watu wanisikilize kweli na wawe na machaguo mengi kwahiyo kuna nyimbo tatu.

Wa kwanza ni ‘sweet song’, wa pili ni wa kidunia kuhusu maisha ‘sensual’ na wa tatu ni wimbo wa kucheza.

Swali: Una nini cha kuwaambia maelfu ya mashabiki wanaosubiri kazi yako mpya?

Charly: Ujumbe ni rahisi nimekuandalia muziki mzuri ambao hautakuchosha, utatoka rasmi Septemba 4, 2021 saa 12:00 jioni. Nenda mtandaoni sikiliza, pakua kwa wingi ili uburudike.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles