BRASILIA, Brazil
WASHAMBULIAJI wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi na Neymar da Silva, wameingia katika vita ya ufungaji bora katika fainali za Kombe la Dunia baada ya wote wawili kupachika mabao manne hadi sasa.
Messi alifunga mabao mawili katika ushindi wa Argentina wa mabao 3-2 dhidi ya Nigeria na kufikisha mabao manne sambamba na mshambuliaji wa Brazil, Neymar amepachika mabao manne baada ya kufunga mawili mechi ya ufunguzi dhidi ya Croatia, kisha kuongeza mawili katika ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Cameroon.
Nyota wengine wanaonyukana kuwania nafasi ya ufungaji bora ni, Arjen Robben, Robin van Persie, James RodrÃguez, Enner Valencia, Karim Benzema na Thomas Müller.