27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Maya: Nami nazeeka bila kupata mtoto

NA RHOBI CHACHA
BAADA ya mwigizaji Wema Sepetu kuweka wazi juu ya masikitiko yake ya kutopata mtoto licha ya kumtafuta kwa muda mrefu, mwigizaji mwingine wa Bongo Movie, Mayasa Mrisho ‘Maya’ naye ameibuka na kudai kwamba anazeeka bila kupata mtoto.
Maya alisema wasanii wenzake wana watoto na wengine wajawazito, lakini yeye bado hajabarikiwa kupata mtoto, jambo linalompa hofu ya kuzeeka bila mtoto.
“Nazeeka bila mtoto wa kumzaa, hapa namuomba Mungu aniwezeshe na kunifungulia uzazi niweze kupata motto, maana umri unakwenda, nitazeeka bila ya kuwa na mtoto jamani,’’ alisikitika Maya.
Kutokana na kauli hiyo, Maya anakuwa mwigizaji wa pili kuweka wazi ya moyoni mwake ya kutokuwa na mtoto na nguvu zao wamezielekeza katika maombi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles