
NA BEATRICE KAIZA,
MTAYARISHAJI wa muziki nchini, Joseph Kimario ‘Master Jay’, ametangaza kufunga ndoa na mpenzi wake wa miaka 10, Sara Kaisi ‘Shaa’ kwa madai kwamba anastahili kuwa mke wake.
Akizungumza na MTANZANIA, Master J alimwelezea Shaa kuwa atakuwa mke bora kwake kwa kuwa ameishi naye muda mrefu hivyo anamjua vizuri.
“Miaka 10 niliyoishi naye nimemwelewa vizuri, anastahili kabisa kuitwa mke wa Master J hapa nafanya taratibu za kumuoa ili tuishi maisha ya mke na mume,” alieleza Master J.
Master J alifafanua zaidi kwamba anampenda Shaa kwa sababu ni msichana anayejielewa, licha ya kuwa msanii hasahau jamii inayomzunguka huku akijituma sana katika kazi zake zote kwa ujumla.