25 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Master J: Nafanya taratibu nimuoe Shaa

Master Jay akiwa na Shaa
Master Jay akiwa na Shaa

NA BEATRICE KAIZA,

MTAYARISHAJI wa muziki nchini, Joseph Kimario ‘Master Jay’, ametangaza kufunga ndoa na mpenzi wake wa miaka 10, Sara Kaisi ‘Shaa’ kwa madai kwamba anastahili kuwa mke wake.

Akizungumza na MTANZANIA, Master J alimwelezea Shaa kuwa atakuwa mke bora kwake kwa kuwa ameishi naye muda mrefu hivyo anamjua vizuri.

“Miaka 10 niliyoishi naye nimemwelewa vizuri, anastahili kabisa kuitwa mke wa Master J hapa nafanya taratibu za kumuoa ili tuishi maisha ya mke na mume,” alieleza Master J.

Master J alifafanua zaidi kwamba anampenda Shaa kwa sababu ni msichana anayejielewa, licha ya kuwa msanii hasahau jamii inayomzunguka huku akijituma sana katika kazi zake zote kwa ujumla.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles