26.3 C
Dar es Salaam
Wednesday, September 18, 2024

Contact us: [email protected]

Klabu 14 zinachuana kuogelea mashindano ya Taifa

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

Jumla ya klabu 14 kutoka Tanzania, Kenya na Uganda zinashuana katika mashindano ya Wazi ya Taifa yanayoendelea kwenye Bwawa la kuogelea la Shuke ya Kimataifa Tanganyika (IST), Masaki, jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo yanahusisha vijana mwenye umri kuanzia miaka 9-23, lengo likiwa nin kupunguza muda wao.

Akizungumzia mashindano hayo ya siku mbili yanayofikia tamati kesho, Mwenyekiti wa Chama cha mchezo wa kuogelea Tanzania( TSA) David Mwasyoge , amesema mchezo huo kwa sasa unashika kasi na amefurahishwa na viwango vilivyoonyeshwa na waogeleaji wanaoshiriki.

“Shindano hili limekuwa na ubora mkubwa kutokana na ongezeko kubwa la waogeleaji tofauti na ukilinganisha na mashindano yaliyofanyika siku za nyuma, amesema Mwasyoge.

Amesema waogeleaji wanaoshindana hapo wale ambao wamekidhi vigezo vya ushiriki wa Kimataifa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles