23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Kenyatta ayajia juu mataifa ya nje

NAIROBI, KENYA

RAIS Uhuru Kenyatta amefungua rasmi kongamano la magavana kujadili mikakati ya kuboresha uchumi jijini Nairobi.

Katika hotuba yake, Rais Uhuru Kenyatta ametupia kidole cha lawama nchi za nje juu ya kile alichosema ni kujaribu kuingilia na kuelekeza Kenya namna ya kuendesha shughuli zake.

Kiongozi huyo wa nchi amesema, Kenya inashukuru uungwaji mkono na ushirikiano inayopata kutoka kwa nchi nyingine lakini nchi yake haitakubali kulazimishwa cha kufanya na yeyote yule.

“Tunashukuru maofisa wa Umoja wa Mataifa na washirika wengine wa maendeleo ambao wamekuwa karibu sana lakini hadi kufikia sasa lazima niweke wazi, wakati tunawashukuru kwa ushirikiano wenu na kutarajia ushirikiano zaidi, lazima mkumbuke Kenya ina wenyewe na wenyewe ni Wakenya milioni 50,” amesema Kenyatta.

Aidha, Rais Uhuru Kenyatta aliwaomba kujizuia kujaribu kuwaelekeza cha kufanya na njia ya kufuata.

“Tunakoelekea kuko wazi. Tunakuomba ujiunge nasi, utuunge mkono katika juhudi zetu hizo. Lakini usiingilie kwasababu hatutakuruhusu uamuru njia tunayostahili kufuata. Nawaomba kwa heshima kubwa mtuheshimu ndipo tutakapo waheshimu. Kila mtu yuko na shida zake hata wao wana shida zao wanazohitajika kuzitatua huko kwao. Nasema hivyo kwa nia njema tu. Sitaruhusu hilo na kama nchi hatutaruhusu hilo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles