MKALI wa muziki wa hip hop, Kandrick Lamar, amemuaga nyota wa kikapu nchini humo, Kobe Bryant, kwa wimbo maalumu.
Bryant anatarajia kutangaza kustaafu mchezo wa kikapu leo baada ya kuutumikia kwa miaka 20 akiwa na timu yake ya Los Angeles Lakers.
Lamar ameamua kutunga wimbo kwa ajili ya kumuaga mchezaji huyo ambaye amefanya makubwa katika mchezo huo.
“Kobe amefanya makubwa katika kikapu, amewafanya watu wapende mchezo huo, kustaafu kwake kutaacha pengo kubwa katika timu ya Lakers japokuwa wapo wachezaji wenye uwezo mkubwa. Kwa kutambua mchango wake nimeona bora nimuage kwa wimbo, kwa heri Kobe,” aliandika kwenye akaunti ya Twitter.