26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Huddah: Kwa sasa mimi ni tajiri

huddah...NAIROBI, KENYA

MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amejitapa na utajiri alionao kwa sasa na kusema kwamba uji wa chumvi aliwahi kunywa mara moja katika kumbukumbu za maisha yake.

Mrembo huyo mwenye mbwembwe nyingi, amedai kwa sasa yeye ni tajiri tofauti na miaka ya nyuma ambayo aliwahi kunywa uji wa mahindi uliowekwa chumvi.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, mrembo huyo aliweka picha huku akionyesha vitu vyake vya thamani, ikiwemo gari lake aina ya Range Rover SUV na nyumba yake mpya.

“Katika maisha hakuna kukata tamaa, ninaamini juhudi zangu zimenifikisha hapa kwa sasa, nina vitu vingi vya thamani kwa sasa na nishasahau maisha yale ya uji wa chumvi.

“Kwa sasa siwezi tena kunywa uji wa mahindi wenye chumvi, niangalie kwa sasa nakula soseji, mikate na vitu vingine,” alieleza Huddah.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles