25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Huawei yasisitiza msimamo wake kuendeleza utandawazi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Kampuni ya Huawei imeahidi kuzingatia mkakati wake wa utandawazi licha ya shinikizo la nje.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Ren Zhengfei ametoa wito kwa utawala mpya wa Marekani kuja na sera za wazi zaidi ambazo ni kwa masilahi ya kampuni za Marekani na uchumi wa Marekani kwa ujumla.

 Hii ni kauli ya kwanza kutolewa na mwanzilishi huyo wa Huawei tangu mabadiliko ya utawala wa Marekani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huawei, Ren Zhengfei.

Ren alikuwa akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Taiyuan, mji mkuu wa mkoa wa kaskazini mwa China wa Shanxi, baada ya kuzindua Maabara ya Ubunifu wa Madini.

“Biashara inanufaisha pande zote mbili. Kuruhusu kampuni za Marekani kusambaza bidhaa kwa wateja wa China ni nzuri kwa utendaji wao wa kifedha. Ikiwa uwezo wa uzalishaji wa Huawei utapanuka, kampuni za Marekani zinaweza kuuza zaidi. Sote tutanufaika. Ninaamini utawala mpya utapima masilahi haya wanapofikiria sera zao, ”amesema Ren.

Ren amesema kuwa Huawei inajenga thamani kwa ekolojia nzima na uchumi mpana. Alitoa mfano kwamba kampuni hiyo imeunda mitandao ya 5G katika miji mingi huko Ulaya, Asia na Mashariki ya Kati, na majaribio ya mtandao huo yamekuwa na ufanisi wa hali ya juu, huku ikifaidisha watumiaji wote kwenye mitandao hiyo.

“Ukweli kwamba watumiaji wa hali ya juu wanaweza kutumia iPhone 12 kikamilifu kwenye mitandao yetu ya 5G huko Ulaya ni ushahidi wa ubora wa mitandao yetu.

 “Kama binadamu tunavyoendelea kufanya maendeleo, hakuna kampuni inayoweza kukuza tasnia ya utandawazi peke yake. Tunahitaji juhudi za pamoja duniani kote,” amesema Ren.

Serikali ya Marekani imekuwa ikifanya kampeni dhidi ya Huawei katika miaka miwili iliyopita ikidai vifaa vya Huawei vinaweza kutumiwa kupeleleza Wamarekani, bila kuwasilisha ushahidi wowote.

Huawei amekataa mara kwa mara madai hayo, na nchi zingine chache zimekubali shinikizo la Marekani, na zinalenga zaidi kuhakikisha wafanyabiashara wote wanakidhi viwango vya kiufundi kwa usalama. 

Ren amesema sasa anajiamini zaidi juu ya uhai wa Huawei kuliko ilivyokuwa awali; “Tumepata njia mpya zaidi za kushinda changamoto zetu. Mapato na mauzo yetu mwaka 2020 yalikuwa makubwa kuliko miaka iliyopita,” Ren aliwaambia waandishi wa habari.

 Kuwezesha mabadiliko ya kidigitali kwa viwanda

Ren alisema mikakati mpya ni pamoja na utafiti na maendeleo na kukuza sekta ya viwanda ulimwenguni kote kuwezesha mabadiliko ya kidigitali na uwezo wake wa msingi wa TEHAMA ya Huawei. Ren pia alisema Maabara ya kisasa ya Ubunifu wa Madini itasababisha huduma bora kwa migodi kwa kutumia teknolojia ya 5G. 

“Kwa kusaidia tasnia ya madini, tunaweza kukuza biashara yetu na kusaidia uzalishaji bora na salama katika migodi. Tunaweza pia kuwezesha wafanyakazi wa mgodi wa makaa ya mawe ‘kuvaa suti na tai’ kazini.

“Katika zama za 5G, kuunganisha biashara ndio lengo kuu. Kuna tasnia nyingi ambazo hatujui sana, kama viwanja vya ndege, bandari, madini ya makaa ya mawe, uzalishaji wa chuma, utengenezaji wa magari, na utengenezaji wa ndege. Ndio maana tuliunda maabara za pamoja ili kujifunza zaidi juu ya mahitaji ya tasnia hizi,” amesema Ren.

Matokeo ya biashara ya Huawei kwa miezi tisa ya kwanza ya mwaka 2020 yalionyesha kuwa, mapato yalikuwa jumla ya yuan bilioni 671.3 (Sawa na dola bilioni 98.57), ongezeko la 9.9% kutoka ile ya kipindi hicho hicho kwa mwaka 2019. 

“Tutaendelea kuwahudumia wateja wetu vizuri kwa kuwajengea thamani zaidi. Tunataka wawe na imani ya kudumu ndani yetu, na tunatumai kuwa hawatayumba kwa sababu ya shinikizo la kisiasa, ” amehitimisha Ren.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles