24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Dogo Janja: ‘My life’ utanitoa upya kimuziki

Dogo-janja-HERIETH FAUSTINE NA RUTH MNKENI

MSANII wa miondoko ya hip hop, AbdulAzizi Abubakari ‘Dogo Janja’, amesema aina ya muziki aliofanya kwenye wimbo wake mpya wa ‘My life’ umelenga kumrudisha kwenye muziki baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu.

Dogo Janja alipata umaarufu kupitia wimbo wa ‘Anajua’ aliomshirikisha Madee.

“Kitu kilichonifanya nibadili uimbaji ni mtayarishaji  Cal kutoka Norway, alinitumia mdundo nilipokwenda studio nikapata melody pamoja na mistari, baada ya hapo nikaupeleka kwa uongozi ndiyo ikawa hivyo ilivyokuwa,” alisema Dogo Janja.

Wakati huo huo, Kampuni ya Lufedha Film inatarajia kutoa filamu yake mpya ijulikanayo kwa jina la ‘Digital Pastor’, yenye mafundisho juu ya elimu ya dini.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Salehe Hamisi ‘Lufedha’ alisema filamu hiyo ni ya 10 na itaanza kusambazwa Machi 7 mwaka huu sehemu mbalimbali za nchi.

Filamu nyingine zilizotolewa na kampuni hiyo ni ‘Sindano ya moto’, ‘Ndoa ya utata’, ‘Mafuriko’ na ‘Mume bora’

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles