30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Diamond, Ali Kiba wachuana Tuzo za Watu

kiba na diamondNA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
WANAMUZIKI mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ na Ali Kiba, ni miongoni mwa wasanii wanaochuana katika Tuzo ya Msanii Bora wa Kiume katika Tuzo za Watu 2015.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Bongo 5 Media Group, inayoratibu tuzo hizo, Nancy Sumari, wasanii wengine walio katika kipengele hicho ni Elias Barnaba, Ommy Dimpoz na Jux.
Katika kipengele cha msanii bora wa kike wanaochuana ni Lady Jaydee, Linah, Mwasiti, Shilole na Vanessa Mdee.
Filamu ya Chausiku, Kigodoro, Madam, Mshale wa Kifo na Sunshine zinashindana kwenye kipengele cha filamu zinazopendwa.
Msanii JB na Ray, wanachuana katika kipengele cha mwongozaji bora wa filamu sambamba na Leah Mwendamseke, Timothy Conrad na William Mtitu.
Alisema Jumamosi yatatangazwa majina ya tano bora na Mei 8 mwaka huu yatatangazwa majina ya waliotinga tatu bora ambapo fainali itafanyika Mei 22.

- Advertisement -

Related Articles

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles