24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

CUBA YATANGAZA SIKU TISA KUMUOMBOLEZA CASTRO

HAVANA, CUBA


fidel-castroWACUBA wameanza kipindi cha siku tisa za maombolezi ya aliyekuwa rais wao na kiongozi wa mapinduzi nchini hapa, Fidel Castro.

Mdogo wake, ambaye ndiye aliyemrithi urais, Raul amesema mwili wa kaka yake aliyefariki juzi utachomwa moto kwa utashi wa kiongozi huyo.

Majivu  ya  Castro  yatazikwa  katika  mji  wa  Santiago de Cuba baada ya siku nane za maombolezi ya  kitaifa yatakayohitimishwa Desemba Nne.

Umma  utaruhusiwa  kushuhudia  mwili  wa  Castro leo na kesho katika  eneo  la  makumbusho  la  Jose Marti  mjini Havana kabla ya kufanyika sala maalumu ya kumuaga kwenye uwanja  mkuu wa mapinduzi mjini  hapa.

Gwaride la nchi nzima litafuatia katika muda wa siku  nne, kwa matembezi ya kilometa 900, na  mkutano  mkubwa wa pili wa sala maalumu utafanyika Jumamosi.

Maafisa  wa  Cuba wamesema tukio la mazishi  linatarajiwa kufanyika  katika makaburi  ya  Santa Ifigenia  mjini  Santiago, Desemba Nne.

Katika  kipindi cha maombolezi  hakutakuwa  na  shughuli au matamasha  ya  wazi, bendera  zitapepea  nusu  mlingoti katika  majengo  ya  serikali huku radio  na  televisheni  zikitarajia kutangaza vipindi  vya  taarifa, uzalendo  na  historia, maafisa  wamesema.

Picha  za  hivi  karibuni  zilizochapishwa  za  Fidel Castro  zilitoka  Novemba  15 mwaka huu wakati alipokutana na Rais wa Vietnam,  Tran Dai Quang.

Na tukio  lake  la  mwisho  kuonekana  hadharani  lilikuwa Agosti 13 katika  ukumbi  wa  matamasha  wa  Karl Max  mjini hapa.

Tangu  alipoondoka madarakani mwaka 2006, Fidel Castro alijing’atua kutoka katika siasa.

Afya  ya  Castro  iliwekwa  siri  kwa  kiasi kikubwa  nchini Cuba na hadi sasa hakuna  taarifa  iliyotolewa  kuhusu sababu  za  kifo  chake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles