31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

CRDB yatangaza neema vitambulisho vya Machinga

Eliya Mbonea, Arusha

Benki ya CRDB imeahidi kuwasimamia vizuri wajasiriamali wadogo (Machinga) waliopewa vitambulisho na serikali ili wainuke kimtaji.

Kauli hiyo imetolewa mjini Arusha na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, katika semina iliyotolewa na benki hiyo kwa wajasiriamali.

“Hii ni fursa kuwatambua wajasiriamali waliopewa vitambulisho, tutawasimamia ili tuwainue kimtaji, Serikali ikimwamini mtu CRDB ni nani tusimwamini na kumhudumia,” amesema Nsekela.

Kwa upande Gambo amewashukuru wafanyabiashara walioshiriki semina hiyo iliyolenga kuwafundisha masuala ya huduma za kifedha zitolewazo na benki hiyo.

“Napongeza juhudi hizi, hili ni kundi muhimu katika kutimiza adhma ya Rais Dk. John Magufuli ya kujenga Tanzania yenye uchumi wa kati wenye kutegemea viwanda, yaani “Tanzania ya viwanda,” amesema Gambo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles