MSANII wa miondoko ya hip pop, Claudia Lubao ‘Chemical’, amefunguka kuwa aliingia kwenye fani hii mara baada ya kumuona msanii, Young D akifanya vizuri kwenye tasnia hiyo.
Alisema msanii huyo alikuwa na umri mdogo lakini mashairi yake yalikuwa na akili nyingi kiasi kwamba alikuwa kivutio kwa wengi jambo ambalo lilimhamasisha naye akaingia katika muziki huo kwa kasi.
“Mimi na Young D tupo sawa kiumri, nikaona hata mimi naweza kufanya kama yeye anavyofanya ndiyo maana nikaamua kuingia kwenye tasnia hii ili niweze kuwaonyesha Watanzania kwamba hata wasichana tunaweza hip pop kama wavulana wanavyoweza,” alieleza.
Msanii huyo ana lengo la kuitangaza zaidi hip hop kimataifa kama wakali mbalimbali wa muziki huo wanavyofanya akiwemo Joh Makini ambaye ndiye msanii anayemvutia katika muziki huo.