31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

CHARUGAMBA AMMWAGIA SIFA ROSE MHANDO

NA CHRISTOPHER MSEKENA

MWIMBAJI wa nyimbo za Injili, Ussy Charugamba, amesema katika wakongwe kwenye tasnia hiyo, anamkubali zaidi Rose Mhando kwa kuwa amewaonyesha njia waimbaji wengi.

Bosi huyo wa Ussy Production, ameliambia MTANZANIA kuwa anajiona mwenye bahati kufanya kazi na Rose Mhando kwa kumshirikisha kwenye wimbo wake unaoitwa ‘Wema’ ambao utakuwa kwenye albamu yake ya sita.

“Rose Mhando ana mchango mkubwa kwenye tasnia hii, amefungua milango kwa waimbaji wengi kufanya hiki wanachokifanya sasa, binafsi najiona mwenye bahati na ninajivunia kufanya kazi na mkongwe huyu, naomba tumpe heshima yake,” alisema Charugamba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles