23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Burundi yatakiwa kusogeza mbele uchaguzi

Burundi's President Pierre NkurunzizaNA SHABANI MATUTU, DAR ES SALAAM

JUMUIYA ya Nchi za Afrika Mashariki (EAC), zimeitaka Burundi kusogeza mbele muda wa uchaguzi kwa mwezi mmoja na nusu ili kurejesha hali ya usalama nchini humo.

Uamuzi huo umefikiwa jana jijini Dar es Salaam na kusomwa na Katibu Mkuu wa EAC, Dk. Richard Sezibera kwa niaba ya wakuu wa nchi za Afrika Mashariki, akisema utasaidia kupunguza vurugu zilizokuwa zikiendelea nchini humo.

Burundi ilikuwa imepanga kufanya uchaguzi wa wabunge wiki ijayo na wa rais Juni 26.

Uamuzi mwingine umezitaka nchi za EAC kuisaidia Burundi kurejesha wananchi wake waliokuwa wamekimbilia huko kutokana na machafuko yaliyotokea.

Pia EAC imetoa wito kwa pande mbili zinazohasimiana kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani ili kudumisha demokrasia nchini humo.

Wakati mkutano huo ukiendelea ripoti zinasema kuwa ofisa mmoja wa Tume ya Uchaguzi ameiambia redio moja ya Ufaransa kuwa ofisa mwenzake, Spes Caritas Ndironkeye hajulikani alipo tangu Ijumaa.

Hata hivyo duru zinaeleza kuwa huenda ofisa mwingine akajiondoa na hivyo kusababisha shughuli za tume hiyo kuzorota.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles