26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

BLACK CHYNA APEWA MSAADA WA KUTEMBEA

Los Angeles, Marekani

MNENGUAJI maarufu nchini Marekani, Black Chyna, jana alionekana jijini Los Angeles, Marekani akitembea kwa kutumia msaada maalumu wa baiskeli ya walemavu.

Hata hivyo, haikuwa wazi sababu za mwanadada huyo ambaye alikuwa na uhusiano na Rob Kardashian, kuomba msaada huo ambao hutolewa kwa watu wenye matatizo maalumu.

Lakini muda mfupi baada ya kupatiwa msaada huo, Black Chyna alionekana akinyanyuka na kutembea hadi lilipo gari lake, jambo ambalo liliwaacha na mashangao watu waliokuwa wakifuatilia tukio hilo.

Tukio hilo lilitokea siku chache baada ya mwanamitindo huyo kuweka wazi kuwa ana mipango ya kutaka kuingia kwenye muziki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles