23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

BIEBER, SELENA WATINGA KANISANI

LAS VEGAS, Marekani


MAPENZI ya staa Justin Bieber na mrembo Selena Gomez yameonekana kukolea, kwani safari hii wameonekana wakihudhuria ibada kanisani.

Wawili hao walinaswa na kamera za mapaparazi wakihudhuria ibada ya jioni ingawa kila mmoja aliingia kivyake, ikiwa ni njia ya kukwepa usumbufu kutoka kwa waandishi wa habari.

Taarifa hiyo ni baada ya ile ya aliyekuwa mpenzi wa Selena, The Weekend, kufuta picha zote za mrembo huyo kwenye akaunti yake ya Instagram.

Weekend mwenye umri wa miaka 27, alikuwa anatoka na Selena (25) lakini msichana huyo ameachana naye na kuamua kurudiana na Bieber aliyewahi kuwa mpenzi wake huko nyuma.

Mbali na Bieber na Selena, staa mwingine aliyefika kanisani siku hiyo alikuwa ni Kourtney Kardashian ambaye ni ndugu wa mke wa Kanye West, Kim Kardashian.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles