24.4 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Balaa la Diamond Sudan Kusini usipime, kiingilio tu utakimbia

NA CHRISTOPHER MSEKENA

STAA wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ameendelea kudhihirisha ubora wake nje ya mipaka ya Bongo baada ya kupiga shoo ya watu maalum usiku wa Krismasi huko, Juba, Sudan Kusini.

Diamond ambaye alikuwa na shoo mbili nchini humo, amefanikiwa kujaza onesho lake la kwanza la watu maalum licha ya kiingilio kuwa kikubwa kilicholipwa kwa dola za Marekani.

Taarifa zinadai katika onesho hilo la watu maalum, kiingilio kwa watu VVIP kilikiwa ni dola za Marekani 1,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni mbili za kibongo, VIP walilipa dola 300 sawa na laki sita viingilio vya kawaida ilikuwa ni dola 100 ambazo ni zaidi ya shilingi laki mbili huku akitarajia kupiga shoo nyingine usiku wa Boxing Day.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles