24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Bagamoyo kumpata Miss Bomba leo

MTZ Alhamisi new july.inddNA PATRICK MWILLONGO, BAGAMOYO

WILAYA ya Bagamoyo, mkoani Pwani, inatarajia kumpata mlimbwende katika shindano la IPAM Mrembo Bomba,
linalotarajiwa kufanyika leo usiku katika ukumbi wa Sky Light, wilayani hapa.

Muandaaji wa shindano hilo, Abdallah Mtangwelah wa kampuni ya Tangwe Man Entertainment, aliwataja warembo wanaowania taji hilo kuwa ni Kalisa Anderson, Katrina John, Fatuma Kassimu, Lulu John na Mariamu Peter.

Wengine ni Salama Jonson na Lulu William, ambao walikuwa wakinolewa na aliyewahi kuwa mshiriki wa shindano la Miss Tanzania Kanda ya Mashariki na Miss Red Valentine, Faith Msuya.

Mkurugenzi Mtendaji wa IPAM Tours, Halid Mjewa, alisema mshindi wa kwanza atapata seti ya televisheni inchi
22 na feni, wa pili atajipatia televisheni inchi 22, wakati wa tatu na nne watapata meza ya mapambo (dressing table), huku mshindi wa tano akipata feni.

- Advertisement -
Previous article
Next article

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles