30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Azam yaisoma Esperance Tunisia

azam web_0NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM

AZAM FC wameanza mikakati kabambe ya kuwamaliza wapinzani wao timu ya Esperance ya Tunisia katika hatua ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho, baada ya kuifanyia ‘ushushushu’ kwa kuwasoma ‘live’ katika mchezo wao wa Ligi Kuu uliochezwa juzi nchini humo.

Esperance wanaoshika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, walitoa kipigo cha bao 2-1 dhidi ya vibonde Club African wanaoshika nafasi ya 11, mchezo ambao ulishuhudiwa na kocha msaidizi Denis Kitambi na Ofisa Mtendaji Mkuu, Saad Kawemba.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kawemba alisema wapo jijini Tunis kuwasoma wapinzani wao, pia kuandaa mazingira watakapofikia wachezaji pindi timu itakapowasili nchini humo kwa mchezo wa marudiano.

“Tulichokuwa tunataka ni kuangalia namna gani wanacheza wakiwa katika mchezo wa ushindani kama tulivyowaona kwenye mechi ya ligi jana (juzi), hata hivyo tutaendelea kuwatazama kupitia kwenye  video tulizonazo ili kuendelea kuwasoma kimbinu.

“Katika mchezo wao huo dhidi ya Club African, tulishuhudia wachezaji wawili wa timu hiyo wakipewa kadi nyekundu, hali inayotupa tahadhari kwamba tukicheza nao kuwe na nidhamu ya kimchezo,” alisema Kawemba.

Akieleza nini wamejifunza kutokana na mchezo huo, Kawemba alisema uzito wa mechi ya Tunisia, utategemea zaidi matokeo ya mchezo wa kwanza utakaochezwa Dar es Salaam Jumapili hii.

“Kwa ufupi kwa matokeo yoyote Dar es Salaam mechi bado haitakua imekwisha, matokeo ya michezo miwili ni muhimu sana,” alisema.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles