23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Anthony Sky kutoa albamu ‘LOUDA’ Machine 26

STOCKHOLM, SWEDEN

Kutoka lebo ya Real Definition Music yenye makazi yake nchini Uingereza (UK), msanii wa Kimataifa wa Afro Pop na Afrobeat, Anthony Sky, amesema ataachia albamu yake inayoitwa LOUDA, Machi 26, mwaka huu.

Msanii huyo mwenye asili ya Nigeria anayeishi Stockholm Sweden, amesema kuwa katika albamu hiyo itakuwa na nyimbo nyingi huku mbili akiwashirikisha mastaa wa Bongo Fleva.

“Unaweza kupata muziki wangu kwenye majukwaa yote ya muziki kama YouTube, Spotify, Boomplay Music, Audiomack na mingine mingi pia mimi nataka kuungana na kuunganisha zaidi Tanzania na Nigeria ndio maana nina miradi mikubwa ya muziki inakuja hivi karibuni ulimwenguni, wakati huu tunasubiria albamu ya LOUDA unaweza kunifuatilia kwenye Instagram yangu kama @iamanthonysky na chaneli yangu ya YouTube ya Anthony Sky,” amesema msanii huyo anayetamba na wimbo, Balancia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles