Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 26 ambaye ni bingwa wa Olimpiki, anaamini ana kila sababu ya kupigana na Fury.
“Ili niweze kutetea mataji yangu lazima nipigane na watu wenye uwezo, ninaamini kwa sasa naweza kupigana na Fury na nikashinda, ninaheshimu uwezo wake lakini katika ugumu chochote kinawezekana.
“Ubingwa wa IBF umezidi kunipa nafasi nzuri ya kupambana katika michezo mingine, hivyo naweza kusema nipo tayari kupambana na bondia huyo mwenye jina kubwa kwa sasa,” alisema Joshua.