30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

ALI KIBA ATIKISA KIGALI

NA BRIGHITER MASAKI


STAA wa Bongo Fleva, Ali Kiba, juzi alitikisa Jiji la Kigali nchini Rwanda kwa kufanya tamasha kali la kufungua mwaka.

Tamasha hilo la ‘East African Party 10’ ambalo lilifanyika katika Uwanja wa Taifa wa mpira wa miguu nchini Rwanda maarufu kama Amahoro, Ali Kiba alijaza watu kwenye uwanja huo.

Ali Kiba alitumbuiza nyimbo zake nyingi za zamani ikiwemo Mac Muga, Cinderella, Nakshi Mrembo na wimbo wake mpya ukiwemo Sedece Me.

Mkali huyo ambaye hivi karibuni aliomba radhi kwa mashabiki zake nchini kwa kutokufanya tamasha la Funga mwaka na Kiba, hatimaye amefungua mwaka nchini Rwanda na kukosha nyoyo za mashabiki wake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles