25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

ALI KIBA ADONDOSHA ZAWADI MBILI

Na SWAGGAZ RIPOTA

BAADA ya kusheherekea siku ya kumbukumbu za kuzaliwa kwake, mfalme wa Bongo Fleva, Ali Kiba wiki hii amewapa zawadi mbili mashabiki wake ambapo kwanza ametoa wimbo unaoitwa Maumivu Per Day pamoja na kumtambulisha, Abdulkiba kupitia lebo yake ya Kings Music.

Katika kuile kinachoonekana kuwakumbusha mashabiki kule ambapo muziki wetu umetokea, Ali Kiba ametumia uwezo wake wa uandishi na sauti maridhawa kunogesha wimbo wa Maumivu Per Day alioutoa kama zawadi ukiwa na mahadhi ya Bongo Fleva ya kitambo.

Na wakati huo huo amemurudisha kwa kishindo mdogo wake, Abdukiba kupitia lebo ya Kings Music kwa kuanchia ngoma  inayoitwa Single, ambapo nyimbo zote hizo mbili zimepokewa vizuri na mashabiki hasa kwenye mtandao wa YouTube.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles