24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Abiria watishia kuchoma moto treni Dar

city-commuter-train

Na Willbroad Mathias, DAR ES SALAAM

TRENI ya abiria  inayofanya safari zake kati ya Kituo Kikuu  cha Reli na maeneo ya Pugu  Dar es Salaam maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ nusura ichomwe moto juzi, baada ya wananchi   kudai kuchoshwa na usumbufu wa shirika hilo.

Wananchi hao walitaka warudishiwe nauli zao  kwa kile walichodai Shirika   la Reli Tanzania (TRL)  limeshindwa kuwa na ratiba inayoeleweka.

Tukio hilo lilitokea juzi  saa 3:00 usiku eneo la Majumbasita, baada ya treni hiyo kukaa kituoni hapo kwa muda mrefu bila kuambiwa kuambiwa chochote.

Hali hiyo iliwafanya abiria  kuvamia kituo kidogo cha mawasiliano kilichopo eneo hilo wakitaka warejeshewe  nauli zao vinginevyo wangekichoma moto pamoja na mabehewa ya treni hiyo.

MTANZANIA liliwashuhudia abiria   wakitaka kuingia ndani ya kituo hicho huku wakiwalazimisha wafanyakazi waliokuwapo wawarudishie fedha zao za nauli.

Purukushani hiyo iliyodumu kwa takribani saa  mbili  ilimalizika kwa abiria hao kuvunja vioo vya mabahewa ya treni vipatavyo 30.

Wafanyakazi kuona hivyo walijifungia ndani ya kituo hicho  huku  polisi  waliokuwa wakisindikiza treni hiyo  wakitimua mbio   kunusuru  maisha yao.

Baadhi ya abiria walisema   tangu Ijumaa   iliyopita wamekuwa wakipata usumbufu kwa kukatishiwa tiketi huku treni  ikichelewa na wakati mwingine kutoonekana  kabisa.

Walisema  jambo hilo  limekuwa likiwasababishia hasara na kuwalazimu  kutafuta usafiri mwingine na   kuchelewa kufika  kwenye  majukumu yao.

Rashid Mpalamo mkazi wa Pugu alisema alipanda treni hiyo  saa 2:30 usiku  kwenye Kituo cha Reli Stesheni, lakini baada ya kufika Majumbasita waliambiwa wasubiri kwa kile kilichodaiwa kuwa   treni ya mizigo ilikuwa imeanguka  maeneo ya Pugu.

Meneja wa  kituo hicho, Benedict Kassege alisema  anashangazwa na kitendo cha abiria hao kuwavamia akidai kuwa wao hawahusiki na ukatishaji tiketi bali wanachokifanya ni mawasiliano ya njia hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles