25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 2, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri Mkuu wa Msumbiji akataa kuwapa silaha raia kupambana na wanamgambo

Msumbiji

Waziri Mkuu wa Msumbiji, Carlos do Agostinho, amepinga wito wa kuwapa raia silaha katika jimbo la Cabo Delgado ili kupambana na wanamgambo wa Kiislamu.

Wakazi wa eneo hilo wakati wote wamekuwa wakiomba silaha ili kuvisaidia vikosi vya usalama.

Waziri Mkuu ametupilia mbali mawazo hayo wakati wa kikao cha masuala ya usalama kilichofanyika mji mkuu, Pemba.

Alisema kuwa hatua hiyo itakuwa ‘’hatari na isiyohimilika’’.

Alisisitiza silaha zinapaswa kuwa katika mikono ya ‘’watu wanaofaa’’, akimaanisha vikosi vya ulinzi na usalama na wale wanaowaamini.

Bwana do Rosario amesema raia wanapaswa kuwa na jembe la kulima na ardhi na kalamu ya kuchangia maendeleo ya taifa lao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles