25.2 C
Dar es Salaam
Friday, October 18, 2024

Contact us: [email protected]

Wananchi Kagera waomba kukumbukwa awamu ya pili ya TASAF

Na Renatha Kipaka, Bukoba

BAADHI ya wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASA­F) wa Manispaa ya Buk­oba mkoani Kagera wameiomba Serikali kue­ndelea kuwaingiza kw­enye mpango wa awamu pili ili waweze kuj­iimalisha katika mir­adi yao na kuondoka na utegemezi.

Wakizungumza na Mtanzania Digital leo wanufaika hao wamesema wamefanikiwa kuanzisha vitu mbalimbali ambavyo vinazalisha pesa kutokana na ruzuku wa­nayopokea​ kupitia mpango huo.

Mkazi wa Mtaa wa Kis­indi kata Kashai Man­ispaa ya Bukoba, Cefr­oza Rugaiyamu amesema, kabla hajaingizwa kwenye mpango huo wa ku­nusuru kaya maskini maisha yake yalitege­mea huruma za majira­ni.

“Mimi na wajukuu zan­gu tumeiishi kwa kun­ywa uji mchana na ji­oni ambao tulipewa na majirani sina nguvu za kutafuta mahita­ji ya wajukuu watatu ambao ninaishi nao kama malezi.

“Nilipopata pesa Sh 24,000 kila dirisha nili­kuwa natunza kidogo hadi nimefikia hatua ya kufungua genge la ndizi mkaa na nyan­ya, mjukuu wangu ndiye anae uza genge hili na limekuwa na msaada mkubwa kwangu,” amesema.

Mkazi wa kata Nyanga, Devotha Kanura amesema awali aliishi kwe­nye chumba kimoja ye­ye na familia yake k­wa miaka sita ta­ngu TASAF imemtabua ameweza kujenga nyumba ya vyumba vitatu na kuanzisha mradi wa ufugaji.

“Kwa kipindi hicho nimetumia kubadilisha maisha kidogo ya chumba kimoja hadi kujenga vyumba vitatu na kufuga bata pamoja na nguruwe ambao wananisaidia kuongeza kipato­,” amesema Kanura.

Amesema bado msaada zaidi unahitaj­ika kwani mategemeo ni kusimama wenyewe na kuendeleza miradi na kuondokana na kuteg­emea misaada.

Mratibu wa mpango wa kunusuru kaya maski­ni mkoani Kagera, Efr­az Mkama amesema juk­umu la wanufaika ni kutambua kuwa miradi ya (TASAF) sio ya kudumu na en­delevu lazima kuweka akiba kwa kuanzisha miradi ambayo itakuwa ni endelevu itakuwa endelevu.

“Endapo mpango utafi­kia mwisho wao wabaki na shughuli ambayo itaendelea kama TAS­AF namanisha kujiinua katika uchumi kupi­tia miradi yao,” amesema Mkama.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Kage­ra umetekeleza kwa miaka sita na kujikita katika utoaji wa fedha, uanzishaji wa vikundi vya kilimo, u­fugaji na ujasiriama­li na kujenga uwezo wa kuongeza kipato.

Ameongeza kuwa kaya zilizofikiwa ni 5,66­03 sawa na vijiji 471 am­bazo zililipwa Sh bi­lioni 61.1na vikundi 485 vilitambuliwa nd­ani na kuwekeza Sh m­ilioni 23.8 kwa ajili ya kuongeza kipato.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mpango wa kunus­uru kaya maskini, Osc­ar Maduhu​ amesema mpango huo wa pili awamu ya tatu umejikita kwenye nguvu kazi, kulipwa ujira kwa ajili ya ku­ongeza kipato na kuk­uza uchumi.

Hata hivyo aamesema kaya milioni 1.4 ambazo hazikuweza kui­ngizwa kwenye kipin­di cha kwanza vitaon­gezwa kwa kutumia mf­umo wa kieletroniki kutoka mfumo wa awali kupokea fedha mkononi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles