27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wanaojiita manabii, walimu wamtisha Askofu Shao

ASKOFU Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao.
ASKOFU Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao.

Na Upendo Mosha, Moshi 

ASKOFU Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao, ameshtushwa na baadhi ya watu walioibukaa na kujiita walimu na manabii huku dhamira yao ikiwa ni kuwatapeli wananchi.

Kutokana na hali hiyo Askofu huyo amewaonya waumini kuwa macho ili kuwaepuka watu hao kwani nia yao si njema kwao na taifa kwa ujumla.

Askofu Shao alisema hayo juzi katika ibada maalumu ya uzinduzi wa jengo la Kanisa la Mtaa wa Kimala, Usharika wa Mwangaria, uliopo kata ya Kahe, wilayani Moshi.

Alisema kumekuwa wimbi kubwa la kuibuka kwa madhehebu mbalimbali ya dini nchini na kuongozwa na watu wanaojiita manabii na walimu huku nia yao ikiwa ni kujipatia fedha na si kueneza neno la Mungu kama inavyodhaniwa.

“Watu hao ambao wamekuwa wakijipambanua kuwa wametumwa na Mungu, wamekuwa wakifanya hivyo kwa lengo la kujitafutia fedha za kujikimu katika maisha yao, huku wakipotosha ukweli kuhusu neno la Mungu jambo ambalo ni hatari.

“Nawaomba waumini kusimamia imani zenu ili kuepuka kuyumbishwa kiimani na baadhi ya walimu na manabii wa uongo wenye kujali maslahi yao binafsi badala ya ukweli wa Mungu,” alisema.

Awali kiongozi wa usharika huo, Mchungaji Richard Njau, alisema mradi wa ujenzi wa kanisa hilo umegharimu zaidi ya Sh milioni 58 hadi kukamilika kwake ambapo awali kabla ya kukamilika kwa ujenzi huo waumini walikuwa wakisali na kuabudu chini ya miti.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles