26.2 C
Dar es Salaam
Sunday, October 13, 2024

Contact us: [email protected]

Wananchi Lindi wampongeza Rais Samia kwa bei nzuri ya korosho

Na Mwandishi Wetu, Lindi

Wakulima wa korosho mkoani Lindi wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake katika kuinua bei ya korosho, jambo lililowaletea manufaa makubwa kiuchumi. Wakiwa kwenye mnada wa korosho uliofanyika hivi karibuni, wakulima walieleza kuwa mafanikio haya yanatokana na uwekezaji wa serikali katika sekta ya kilimo, hususan kwa kutoa huduma bora za ugani na ruzuku ya viuatilifu.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima, mmoja wa wakulima hao, Saidi Athumani, alisema kuwa jitihada za Rais Samia zimeleta mwamko mpya katika kilimo cha korosho, ambapo uzalishaji umeongezeka kutokana na msaada wa vifaa bora na elimu kwa wakulima. “Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa msaada mkubwa aliotupa. Tumepata huduma za ugani za kutosha na ruzuku ya viuatilifu ambavyo vimetusaidia kupata mazao bora,” alisema Saidi.

Wakulima hao waliongeza kuwa uboreshaji wa huduma za ugani na upatikanaji wa viuatilifu kwa wakati, umechangia kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo kuboresha faida yao. Kwa mujibu wa taarifa za soko, bei ya korosho imepanda ikilinganishwa na miaka iliyopita, jambo linalodhihirisha matokeo ya juhudi za serikali katika kuimarisha soko la ndani na la kimataifa.

Wakati wa mnada huo, baadhi ya wakulima walionekana wakibeba mabango yenye ujumbe wa shukrani kwa Rais Samia. “Asante Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuinua zao la korosho,” lilikuwa moja ya mabango yaliyoonekana kwenye mnada huo.

Serikali ya Rais Samia imekuwa ikisisitiza umuhimu wa sekta ya kilimo kwa maendeleo ya nchi, na imekuwa ikitoa kipaumbele kwa mazao kama korosho kwa kuwasaidia wakulima kupata mbinu na nyenzo bora. Wakulima wa Lindi wanaamini kuwa jitihada hizi zitawawezesha kuongeza tija katika kilimo na kuinua vipato vyao, huku wakiomba serikali iendelee na juhudi zake ili korosho iendelee kuwa tegemeo la uchumi wa mkoa huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles