27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Waliokimbia kuketetwa, kuolewa wadai kutimiza ndoto za elimu

NA MARY MWITA

BAADHI ya wasichana waliokimbia wakati wakilazimishwa kukeketwa ili wapatiwe wachumba kwa mujibu wa  mila na desturi za kabila zao wamedai wametimiza ndoto zao za kupata elimu.

Walisema kukimbia  ukeketaji kumewapa mwanga wa maisha na kutimiza ndoto zao za kuishi maisha bora  na kudai bado kuna ukatili wa watoto wa kike katika jamii za wafugaji.

Mkazi wa Arumeru, Riziki Meijo alisema akiwa mmoja waathirika wa ukatili wa ukeketaji alikombolewa na Shirika lisilo la kiserikali la Health Integrated Multisectoral  Development (HIMD) na tayari amewezeshwa kufanya shughuli za kiuchumi.

Alisema ukeketaji ni hatari na baadhi ya wasichana waliofanyiwa ukatili huo wameathirika kisaikolojia.

Mkurugenzi  Mtendaji wa HIMD, Mackrine Rumanyika  alisema baadhi ya jamii bado zinafanya ukeketaji na kutaka mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kudhibiti ukatili huo.

Alisema wasichana zaidi ya 100, wamekimbilia na kupewa msaada katika shirika hilo.

Mackrine alisema  wanasaidia wasichana wanaokimbia kwa kuwapatia elimu hadi vyuo vikuu   na kuwa wamekuwa msaada kwa familia zao na kuwa jamii bora kwa wasichana wa jamii zao.

Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 imeendelea kusimamia masilahi mapana ya mtoto bila kubagua jinsi,  na sera ya elimu ya mwaka 2015 imekataza kila aina ya unyanyasaji wa mtoto wa kike na kutambua misingi ya haki na usawa kwa watoto wa kike  na wa kiume.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles