21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Viongozi wa kijiji, wananchi na wahanga wa ujambazi Serengeti watuma salamu kwa IGP

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Leo Septemba 29, 2022 Wakazi wa Kijiji cha Nyamakobiti kilichopo Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara wametuma salamu za Pongezi na Ahsante kwa IGP Wambura na Jeshi lote la Polisi kwa Operesheni mbalimbali za kutokomeza wahalifu Kijijini hapo na maeneo mbalimbali nchini.

Wananchi hao wametuma salamu hizo kupitia mkutano wa hadhara wa wanakijiji ulioandaliwa na viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Nyamakobiti na maeneo ya jirani uliolenga kulipongeza jeshi la Polisi na kuliomba liendelee na operesheni hizo za kudhibiti wahalifu ili kijijini hapo paendelee kuwa sehemu salama na wananchi waweze kufanya shuguli za kujiletea maendeleo bila hofu yoyote.

Aidha, wahanga wa vitendo vya uhalifu katika kijiji hicho wametoa shuhuda mbalimbali kueleza namna walivyoteswa na matukio ya ujambazi kwa kuibiwa mali zao kama vile mifugo, pikipiki pamoja na kujeruhiwa na kuuliwa na Majambazi Sugu kijijini hapo kabla ya Jeshi la Polisi kuwashugulikia kikamilifu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles