24.6 C
Dar es Salaam
Wednesday, June 26, 2024

Contact us: [email protected]

Utamaduni wa asili zao jipya la utalii

Eliya Mbonea, Arusha



Watanzania na wadau wa utalii nchini  wametakiwa kuwekeza katika zao la utalii wa utamaduni wa asili nchini ili kukuza utalii.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Arusha na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Suzan Mlawi alipofungua Tamasha la Urithi Festival kwa niaba ya Waziri Dk. Harrison Mwakyembe.

Tamasha hilo linafanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha likishirikisha tamaduni mbalimbali za makabila yanayopatikana mkoani Arusha.

Akizungumza wakati wa ufunguzi Katibu Mkuu Mlawi amesema, utalii wa utamaduni umekuwa kivutio duniani pote hivyo ni vyema Wadau wa utalii wakautumia kama fursa ya kujiletea maendeleo.

“Utalii wa utamaduni duniani umekuwa kivutio kioya kutokana na jamii nyingi kupoteza utamaduni wao na hivyo kuwafanya watu kusafiri maeneo mbalimbali ili kujifunza tamaduni nyingine,” amesema Mlawi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tamasha hilo, Professa Audax Mabula, amesema, zao hilo jipya la utalii litaongeza ajira na kufungua soko jipya la bidhaa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
588,000SubscribersSubscribe

Latest Articles