33.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, October 22, 2024

Contact us: [email protected]

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Esther Mnyika, Mtanzania Digital

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza kazi rasmi, hivyo kutoa wito kwa wananchi kutoa maoni ya kile wanachohotaji kifanyiwe maboresho katika mfumo wa ulipaji na ukusanyaji kodi.

Akizungumza leo Oktoba, 22 2024 Ikulu jijini Dar es Salaam,  Mwenyekiti wa tume hiyo, Balozi Ombeni Sefue amesema wapo tayari kushirikiana na kumsikiliza kila mdau  iwe mmoja mmoja, kupitia vyama vya kitaalamu, jumuiya za biashara na nyingine ili kupata maoni yatakayowasilishwa kwa Rais Dk. Samia Suluhu.

Balozi Sefue amesema lengo ni kuhakikisha kunakuwa na mfumo bora wa kukusanya mapato na itafanya tathimini hiyo kwa kushirikisha wananchi.

“Mtakumbuka kuwa tarehe 4 Oktoba 2024, Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alizindua rasmi Tume ya Kutathmini na Kushauri kuhusu Maboresho ya Kodi.

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi mara baada ya hafla ya uzinduzi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam Oktoba 04 2024.


Kama mjuavyo Tume hii imeundwa kufuatia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji kuhusu kero mbalimbali zinazotokana na mfumo wa kodi nchini,” ameeleza  Mwenyekiti huyo.

Amefafanua kuwa Tume hiyo imepewa miezi sita lakini machakato wa kutoa maoni utachukua kipindi kisichopungua miezi miwili kuanzia sasa, baada ya hapo watachukua mapendekezo hayo, kuyafanyia tathmini na kuyachanganua kabla ya kuwasilisha kwa Rais.

Ameeleza kuwa wameandaa namna bora ya kuratibu  ushiriki wa wananchi, wafanyabiashara, wawekezaji na taasisi za umma na binafsi, asasi za kiraia, wadau wa maendeleo na wananchi wanaishi nje ya nchi ikiwamo kufanya mikutano katika maeneo mbalimbali.

“Tumeandaa mifumo rahisi, rafiki ya wazi ya ukusanyaji wa maoni kutoka kwa wadau wa aina zote nchini ikiwemo dodoso la mtandaoni linalopatikana kupitia kiunganishi cha edodoso.gov.go.tz kwa kutumia namba ya dodoso 544978, barua pepe [email protected] na maboresho. [email protected], namba za simu 0748 755 677, 0738 588 813,”

Balozi Sefue amesema lengo la Serikali imedhamiria  kufikia kiwango  cha asilimia 15 ya pato la Taifa  ifikapo mwaka 2026/27  hatua itakayoongeza  uwezo wa nchi kugharamia miradi ya maendeleo na kupunguza kiwango cha utegemezi wa mikopo na misaada.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles