30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

SIOGOPI KUFUNGIWA BUNGENI – MCHUNGAJI MSIGWA

Na FRANCIS GODWIN– IRINGA

MBUNGE  wa  Iringa Mjini Mchungaji Peter  Msigwa (Chadema), amesema  ataendelea kusimamia  ukweli na hataogopa  kufungiwa  bungeni.

Alisema ataliambia Bunge na wananchi kwamba hali ya maisha mtaani ni  ngumu  hata kama ukweli huo utasababisha yeye kufukuzwa bungeni.

Alisema kazi ya wabunge kwa ujumla wake ni kuihoji na kuikosoa Serikali hivyo hataacha  kuikosoa  inapofanya tofauti lakini pia haogopi kuchukuliwa hatua na kupewa na Spika wa  Bunge ambaye  hapendi kuona wabunge wa upinzani  wakiikosoa Serikali iliyopo madarakani.

Akiwahutubia wananchi wa Iringa Mjini, katika Uwanja wa Mwembetogwa, Mchungaji Msigwa, alisema  mtaani kuna uhaba mkubwa wa fedha ambao umesababisha watu kukosa fedha mifukoni ambayo imewakumba wabunge pia.

“Kazi yangu kama mbunge si kupongeza kila jambo ila pale Serikali inapokwenda ndivyo sivyo kazi ya Kambi ya upinzani bungeni ni kuikosoa yasiyokwenda sawa.

“Ninaongea haya huku nikijua nitafungiwa ama kupewa adhabu kwa kuyasema haya ila siogopi hata kama nitapewa adhabu ya kufungiwa hata mwaka mmoja poa tu, ila nitasimamia ukweli.

Mchungaji Msigwa alisema anashangazwa na kauli ya Serikali kwamba uchumi wa Tanzania upo juu kuliko nchi yoyote Afrika, lakini ni wakati wa kila Mtanzania kujiuliza kama mfukoni mwake kuna pesa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles