21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Sina haja ya kutumia fedha kumnadi mtu – Lowassa

mNa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

WAZIRI Mkuu wa Zamani Edward Lowassa, amekanusha taarifa zilizochapishwa na gazeti moja la kila wiki iliyosema “Lowassa apanga safu”, akisema hana haja ya kufanya hivyo wala kutumia fedha kumnadi mgombea yeyote.

Taarifa iliyotolewa ofisi yaje jana, ilisema habari hiyo ilijengwa na taswira ya uongo kwamba kuna mpango wa kupanga nani atagombea ubunge katika Jimbo la Monduli baada ya Lowassa kumaliza muda wake.

“Taarifa hiyo potofu ilikuwa na lengo la kumshushia Lowassa hadhi kwa wananchi wake,” ilisema taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taaifa hiyo, Lowassa anatarajia kupeleka malalamiko rasmi kwenye Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Idara ya Habari (Maelezo) ili ukweli ujulikane.

Ilisema habari hiyo ilidai kuwa Lowassa amewahonga makada kadhaa wa CCM wilayani humo ambao wameonyesha au wana nia ya kuwania kiti hicho, Sh millioni 10 kila mmoja ili wamuunge mkono Mbunge wa Viti Maalum, Namelok Sokoine.
Taraifa hiyo ilimnukuu Lowassa akisema, “Huu ni muendelezo wa habari za uongo na uzushi dhidi yangu ambao gazeti hili limekuwa likiufanya kwa muda mrefu sasa. Gazeti hili limekuwa likitumika kama chombo cha propaganda dhidi yangu,” alisema Lowassa na kuongeza:
“Kwa muda mrefu sasa gazeti hili limekuwa likizusha habari za uongo dhidi yangu. Mfano ni taarifa potofu na ovu ya mimi kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kongosho nchini Ujerumani jambo ambalo ni uongo”.
Alisema inasikitisha kuona gazeti lenye waandishi na wahariri makini kama hilo linaweza kuacha kufuata maadili ya uandishi wa habari na kuamua kuandika habari ambazo hazina hata chembe ya ukweli.
“Lazima watambue kwamba wananchi wamekwisha kuelewa uovu na uonevu wa gazeti hili dhidi yangu,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles