23.1 C
Dar es Salaam
Sunday, September 8, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yakiri gereza la Butimba kufurika wafungwa

Na Sheila   Katikula, Mwanza

Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amesema gereza na Butimba lililipo jijini hapa lina idadi kubwa ya mahabusu ni vema kutupia jicho la karibu  ili kuweza kusikili mashauri ya kesi zao na haki itendeke kwa watu hao.

Hayo aliyasema jana  kwenye ziara yake ya Siku moja alipotembelea gereza hilo na kuzungumza na watumishi na wafungwa alisema   gereza hilo lina wafungwa zaidi ya 1000 na mahabusu 760 kasi ya siyo nzuri katika kusikiliza mashauri yaliyopo hasa kwenye  mahakama kuu.

Alisema atahakikisha anazungumza na Waziri wa Katiba na sheria ili waweze kuona haki inatendeka dhidi ya wahumiwa hao. 

“Nimesikiliza changamoto za mashauri kama mnavyofahamu kwenye magereza kuna watu wa mbalimbali  nimeongea nao japo siyo wote  ili niweze kujua mambo yao ambayo hawanahisi hawakutendewa haki  nimeyachukua  nitajalibu kuwasiliana na vyombo husika ili kuhakikisha wanayafanyia kazi masuala hayo ili haki itendeke,” alisema Simbachawene.

 Alisema Serikali ya awamu ya sita imeanza kupunguza baadhi ya changamoto zikiwamo za kununua sare, masilshi madogo madogo na nyongeza zimeanza kutokea kwa mfano fulsa mbalimbali za kupunguza makali ya askari na mengine walitonieleza askari hawa nitayapeleka kwenye mamlaka ili tuweze kuona jinsi ya kuyapunguza,” alisema Simbachawene.

Kwa upande wake Mkuu wa Gereza la Butimba Mkoa Mwanza, Peter Anatory alisema gereza hilo linakaa na wahalifu asilimia 75.18 ambao wametoka sehemu mbalimbali na watumishi waliopo ni asilimia 52.12.

Hata hivyo, Anatory alimshukru Waziri huyo kwa kutembelea gereza hilo na kutoa maelezo kwa wahumiwa na mahabusu hao na kusikiliza changamoto zao.

“Nimefurahi kuona waziri akizungumza na wahalifu hawa na kuwasihi  kuishi kwa amani na  upendo na kuwata kutumikia sehemu ya adhabu kwa walio hukumiwa na mahabusu kuendelea kuwa watulivu ili waweze kusubili mahamuzi ya kimahakama,”alisema Anatory.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles