21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Rick Rose, 50 Cent wazidi kutishana

Rick RoseLAS VEGAS, MAREKANI

RAPA wa kundi la Maybach Music, Rick Rose na kiongozi wa kundi la G Unit, 50 Cent, bifu lao limefikia pabaya baada ya Rick Rose kueleza kwamba 50 Cent amefilisika kimuziki.

50 Cent aliwahi kusema kwamba amefilisika ili asaidiwe ama kufilisiwa mali zake kutokana na madeni anayodaiwa, ndipo Rick Rose alipotumia maneno yake kumshambulia huku akisema kuwa 50 Cent hana kitu na ameanza kufanya biashara ya nguo badala ya kufanya muziki.

Bifu hili limeendelea zaidi huku 50 Cent akidai anao mkanda wa ngono unaomuonyesha mpenzi wa Rick Rose akifanyiwa kitendo hicho.

Hata hivyo wawili hao wameanza kutambiana kwa kushindanisha mali wanazomiliki, huku 50 akidai kwamba mbali na muziki ana biashara mbalimbali ambazo zinamuingizia fedha nyingi kwa mwaka dhidi ya Rick Ross.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles