Mwenyekiti wa Kamisheni wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk. Hedwiga Swai(aliyesimama) akisalimia wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (ATF) na Kamisheni wakati wa kikao cha pamoja chenye lengo la kufahamiana na kujadili shughuli mbalimbali zinaotekelezwa na TACAIDS, kikao hicho kilichofanyika Mei 25, 2022 jijini Dodoma, kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya ATF, Caroline Mdundo na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dk. Leonard Maboko.
Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dk. Leonard Maboko akifafanua lengo la TACAIDS kukutanisha Bodi hizo mbili za ATF na ile ya Kamisheni ambazo zote zinaisimamia Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma Mei 25, 2022
Wajumbe wa Kamisheni, wajumbe wa Bodi ya ATF na Menejimenti walioshiriki kikao cha pamoja kwa lengo la kufahamiana pamoja na kujadili majukumu ya Bodi zote mbili, majukmu ya TACAIDS, muundo na tathimini ya utekelezaji wa Mkakati wa nne (MNSF IV), vipaumbele vya mkakati wa tano wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania(NMSF V) na matokeo yanayotegemewa pamoja na mpango wa utekelezaji wa ATF na Mapendekezo ya kuboresha vyanzo vya fedha vya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI.Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Richard Ngirwa akiwasilisha tathimini ya utekelezaji wa Mkakati wa nne (MNSF IV), vipaumbele vya Mkakati wa tano wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania(NMSF V) na matokeo yanayotegemewa katika kikao cha Kamisheni na bodi ya ATF kilichofanyika tarehe 25Mei,2022 jijini Dodoma.Mjumbe wa Kamisheni ya TACAIDS, Dk. Sajida Kimambo akizungumzia umuhimu wa kutoa kipaumbele kwa huduma za kutokomeza maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka kushoto ni Prof. Magreth Bushesha na kulia kwake ni Bahati Haule. Wote ni makamishina wa TACAIDS.Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI(ATF), Caroline Mdundo akijadili ajenda ya muundo wa TACAIDS baada ya kuwasilishwa na wataalam, wakati wa majadiliano katika kikao hicho kilichokutanisha bodi ya ATF na Kamisheni Mei 25, 2022 jijini Dodoma.